Zab. 102:11-15 Swahili Union Version (SUV)

11. Siku zangu zi kama kivuli kilichotandaa,Nami ninanyauka kama majani.

12. Bali Wewe, BWANA utaketi ukimiliki milele,Na kumbukumbu lako kizazi hata kizazi.

13. Wewe mwenyewe utasimama,Na kuirehemu Sayuni,Kwa maana ndio wakati wa kuihurumia,Naam, majira yaliyoamriwa yamewadia.

14. Maana watumishi wako wameyaridhia mawe yake,Na kuyaonea huruma mavumbi yake.

15. Kisha mataifa wataliogopa jina la BWANA,Na wafalme wote wa dunia utukufu wako;

Zab. 102