1. Rehema na hukumu nitaziimba,Ee BWANA, nitakuimbia zaburi.
2. Nitaiangalia njia ya unyofu;Utakuja kwangu lini?Nitakwenda kwa unyofu wa moyoNdani ya nyumba yangu.
3. Sitaweka mbele ya macho yanguNeno la uovu.Kazi yao waliopotoka naichukia,Haitaambatana nami.
4. Moyo wa ukaidi utaondoka kwangu,Lililo ovu sitalijua.