11. Asema moyoni mwake, Mungu amesahau,Auficha uso wake, haoni kamwe.
12. BWANA, uondoke, Ee Mungu, uuinue mkono wako,Usiwasahau wanyonge.
13. Kwani mdhalimu kumdharau Mungu.Akisema moyoni mwake, Hutapatiliza?
14. Umeona, maana unaangalia madhara na jeuri,Uyatwae mkononi mwako.Mtu duni hukuachia nafsi yake,Maana umekuwa msaidizi wa yatima.