23. na juu ya Kiriathaimu, na juu ya Beth-gamuli, na juu ya Beth-meoni;
24. na juu ya Keriothi, na juu ya Bozra, na juu ya miji yote ya nchi ya Moabu, iliyo mbali na iliyo karibu.
25. Pembe ya Moabu imekatika, na mkono wake umevunjika, asema BWANA. Mlevyeni; kwa maana alijitukuza juu ya BWANA
26. na Moabu atagaa-gaa katika matapiko yake, naye atadhihakiwa. Kwa maana Israeli, je! Hakuwa dhihaka kwako?
27. Alionekana kati ya wevi? Maana kila umtajapo watikisa kichwa chako.
28. Enyi mkaao Moabu, iacheni miji,Enendeni kukaa majabalini;Mkawe kama njiwa afanyaye kioto chakeKatika ubavu wa mdomo wa shimo.
29. Tumesikia habari za kiburi cha Moabu;Ya kuwa ana kiburi kingi;Jeuri yake, na kiburi chake, na majivuno yake,Na jinsi alivyotakabari moyoni mwake.
30. Najua ghadhabu yake, asema BWANA, ya kuwa si kitu; majisifu yake hayakutenda neno lo lote.
31. Kwa sababu hiyo nitampigia yowe Moabu, naam, nitapiga kelele kwa ajili ya Moabu yote; nitawaombolezea watu wa Kir-heresi.