19. Ee binti ukaaye katika Misri,Ujiweke tayari kwenda zako hali ya kufungwa;Kwa maana Nofu utakuwa ukiwa,Utateketezwa, usikaliwe na watu.
20. Misri ni mtamba mzuri sana, lakini uharibifu umekuja,Umekuja utokao pande za kaskazini.
21. Na watu wake waliojiwa, walio kati yake,Ni kama ndama waliowanda malishoni;Maana wao nao wamerudi nyuma,Wamekimbia wote pamoja, wasisimame;Maana siku ya msiba wao imewafikilia,Wakati wa kujiliwa kwao.
22. Sauti yake ni kama nyoka, wajapo kwa nguvu,Watamjia na mashoka, kama wachanja kuni.
23. Wataukata msitu wake, asema BWANA, ingawa haupenyeki;Kwa maana ni wengi kuliko nzige, hawahesabiki.
24. Binti ya Misri ataaibishwa;Atatiwa mikononi mwa watu wa kaskazini.