7. Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea BWANA,Ambaye BWANA ni tumaini lake.
8. Maana atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji,Uenezao mizizi yake karibu na mto;Hautaona hofu wakati wa hari ujapo,Bali jani lake litakuwa bichi;Wala hautahangaika mwaka wa uchache wa mvua,Wala hautaacha kuzaa matunda.
9. Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?
10. Mimi, BWANA, nauchunguza moyo, navijaribu viuno, hata kumpa kila mtu kiasi cha njia zake, kiasi cha matunda ya matendo yake.