Yer. 17:1-7 Swahili Union Version (SUV)

1. Dhambi ya Yuda imeandikwa kwa kalamu ya chuma, na kwa ncha ya almasi; imechorwa katika kibao cha moyo wao, na katika pembe za madhabahu zenu;

2. na wakati huo watoto wao wazikumbuka madhabahu zao, na maashera yao, karibu na miti yenye majani mabichi juu ya milima mirefu.

3. Ee mlima wangu wa uwandani, nitatoa mali zako na hazina zako zote ziwe nyara, na mahali pako palipoinuka, kwa sababu ya dhambi, katika mipaka yako yote.

4. Nawe, naam, wewe nafsi yako, utaachana na urithi wako niliokupa; nami nitakulazimisha kuwatumikia adui zako katika nchi usiyoijua; maana umewasha moto katika hasira yangu, utakaowaka milele.

5. BWANA asema hivi,Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu,Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yakeNa moyoni mwake amemwacha BWANA.

6. Maana atakuwa kama fukara nyikani,Hataona yatakapotokea mema;Bali atakaa jangwani palipo ukame,Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.

7. Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea BWANA,Ambaye BWANA ni tumaini lake.

Yer. 17