Rum. 15:9-18 Swahili Union Version (SUV)

9. tena ili Mataifa wamtukuze Mungu kwa ajili ya rehema zake; kama ilivyoandikwa,Kwa hiyo nitakushukuru kati ya Mataifa,Nami nitaliimbia jina lako.

10. Na tena anena,Furahini, Mataifa, pamoja na watu wake.

11. Na tena,Enyi Mataifa yote, msifuni Bwana;Enyi watu wote, mhimidini.

12. Na tena Isaya anena,Litakuwako shina la Yese,Naye aondokeaye kuwatawala Mataifa;Ndiye Mataifa watakayemtumaini.

13. Basi Mungu wa tumaini na awajaze ninyi furaha yote na amani katika kuamini, mpate kuzidi sana kuwa na tumaini, katika nguvu za Roho Mtakatifu.

14. Ndugu zangu, nimehakikishwa mimi mwenyewe kwa habari zenu ya kuwa ninyi nanyi mmejaa wema, mmejazwa elimu yote, tena mwaweza kuonyana.

15. Lakini nawaandikia, kwa ujasiri zaidi katika sehemu za waraka huu, kana kwamba kuwakumbusha, kwa neema ile niliyopewa na Mungu,

16. ili niwe mhudumu wa Kristo Yesu kati ya watu wa Mataifa, niifanyie Injili ya Mungu kazi ya ukuhani, kusudi Mataifa wawe sadaka yenye kibali, ikiisha kutakaswa na Roho Mtakatifu.

17. Basi, nina sababu ya kuona fahari katika Kristo Yesu mbele za Mungu.

18. Maana sitathubutu kutaja neno asilolitenda Kristo kwa kazi yangu, Mataifa wapate kutii, kwa neno au kwa tendo,

Rum. 15