Omb. 5:9-18 Swahili Union Version (SUV)

9. Twapata chakula kwa kujihatarisha nafsi zetu;Kwa sababu ya upanga wa nyikani.

10. Ngozi yetu ni nyeusi kama tanuu;Kwa sababu ya hari ya njaa ituteketezayo.

11. Huwatia jeuri wanawake katika Sayuni;Na mabikira katika miji ya Yuda.

12. Wakuu hutungikwa kwa mikono yao;Nyuso za wazee hazipewi heshima.

13. Vijana huyachukua mawe ya kusagia;Na watoto hujikwaa chini ya kuni.

14. Wazee wameacha kwenda langoni;Na vijana kwenda ngomani.

15. Furaha ya mioyo yetu imekoma;Machezo yetu yamegeuka maombolezo.

16. Taji ya kichwa chetu imeanguka;Ole wetu! Kwa kuwa tumetenda dhambi.

17. Kwa sababu hiyo mioyo yetu imezimia;Kwa ajili ya hayo macho yetu hayaoni vema.

18. Kwa ajili ya mlima Sayuni ulio ukiwa,Mbweha hutembea juu yake.

Omb. 5