7. Baba zetu walitenda dhambi hata hawako;Na sisi tumeyachukua maovu yao.
8. Watumwa wanatutawala;Hakuna mtu wa kutuokoa na mikono yao.
9. Twapata chakula kwa kujihatarisha nafsi zetu;Kwa sababu ya upanga wa nyikani.
10. Ngozi yetu ni nyeusi kama tanuu;Kwa sababu ya hari ya njaa ituteketezayo.
11. Huwatia jeuri wanawake katika Sayuni;Na mabikira katika miji ya Yuda.
12. Wakuu hutungikwa kwa mikono yao;Nyuso za wazee hazipewi heshima.
13. Vijana huyachukua mawe ya kusagia;Na watoto hujikwaa chini ya kuni.
14. Wazee wameacha kwenda langoni;Na vijana kwenda ngomani.
15. Furaha ya mioyo yetu imekoma;Machezo yetu yamegeuka maombolezo.
16. Taji ya kichwa chetu imeanguka;Ole wetu! Kwa kuwa tumetenda dhambi.