Omb. 5:7-14 Swahili Union Version (SUV)

7. Baba zetu walitenda dhambi hata hawako;Na sisi tumeyachukua maovu yao.

8. Watumwa wanatutawala;Hakuna mtu wa kutuokoa na mikono yao.

9. Twapata chakula kwa kujihatarisha nafsi zetu;Kwa sababu ya upanga wa nyikani.

10. Ngozi yetu ni nyeusi kama tanuu;Kwa sababu ya hari ya njaa ituteketezayo.

11. Huwatia jeuri wanawake katika Sayuni;Na mabikira katika miji ya Yuda.

12. Wakuu hutungikwa kwa mikono yao;Nyuso za wazee hazipewi heshima.

13. Vijana huyachukua mawe ya kusagia;Na watoto hujikwaa chini ya kuni.

14. Wazee wameacha kwenda langoni;Na vijana kwenda ngomani.

Omb. 5