13. Vijana huyachukua mawe ya kusagia;Na watoto hujikwaa chini ya kuni.
14. Wazee wameacha kwenda langoni;Na vijana kwenda ngomani.
15. Furaha ya mioyo yetu imekoma;Machezo yetu yamegeuka maombolezo.
16. Taji ya kichwa chetu imeanguka;Ole wetu! Kwa kuwa tumetenda dhambi.
17. Kwa sababu hiyo mioyo yetu imezimia;Kwa ajili ya hayo macho yetu hayaoni vema.
18. Kwa ajili ya mlima Sayuni ulio ukiwa,Mbweha hutembea juu yake.
19. Wewe, BWANA, unadumu milele;Kiti chako cha enzi ni tangu kizazi hata kizazi.
20. Mbona watusahau sikuzote;Na kutuacha muda huu mwingi?
21. Ee BWANA, utugeuze kwako, nasi tutageuka; Zifanye mpya siku zetu kama siku za kale.
22. Isipokuwa wewe umetukataa kabisa;Nawe una hasira nyingi sana juu yetu.