Omb. 5:13-20 Swahili Union Version (SUV)

13. Vijana huyachukua mawe ya kusagia;Na watoto hujikwaa chini ya kuni.

14. Wazee wameacha kwenda langoni;Na vijana kwenda ngomani.

15. Furaha ya mioyo yetu imekoma;Machezo yetu yamegeuka maombolezo.

16. Taji ya kichwa chetu imeanguka;Ole wetu! Kwa kuwa tumetenda dhambi.

17. Kwa sababu hiyo mioyo yetu imezimia;Kwa ajili ya hayo macho yetu hayaoni vema.

18. Kwa ajili ya mlima Sayuni ulio ukiwa,Mbweha hutembea juu yake.

19. Wewe, BWANA, unadumu milele;Kiti chako cha enzi ni tangu kizazi hata kizazi.

20. Mbona watusahau sikuzote;Na kutuacha muda huu mwingi?

Omb. 5