Omb. 5:1-7 Swahili Union Version (SUV)

1. Ee BWANA, kumbuka yaliyotupata;Utazame na kuiona aibu yetu.

2. Urithi wetu umegeuka kuwa mali ya wageni;Na nyumba zetu kuwa mali ya makafiri.

3. Tumekuwa yatima waliofiwa na baba;Mama zetu wamekuwa kama wajane.

4. Tumekunywa maji yetu kwa fedha;Kuni zetu twauziwa.

5. Watufuatiao wa juu ya shingo zetu;Tumechoka tusipate raha yo yote.

6. Tumewapa hao Wamisri mkono;Na Waashuri nao, ili tushibe chakula.

7. Baba zetu walitenda dhambi hata hawako;Na sisi tumeyachukua maovu yao.

Omb. 5