Omb. 5:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Ee BWANA, kumbuka yaliyotupata;Utazame na kuiona aibu yetu.

2. Urithi wetu umegeuka kuwa mali ya wageni;Na nyumba zetu kuwa mali ya makafiri.

3. Tumekuwa yatima waliofiwa na baba;Mama zetu wamekuwa kama wajane.

4. Tumekunywa maji yetu kwa fedha;Kuni zetu twauziwa.

Omb. 5