1. Ee BWANA, kumbuka yaliyotupata;Utazame na kuiona aibu yetu.
2. Urithi wetu umegeuka kuwa mali ya wageni;Na nyumba zetu kuwa mali ya makafiri.
3. Tumekuwa yatima waliofiwa na baba;Mama zetu wamekuwa kama wajane.
4. Tumekunywa maji yetu kwa fedha;Kuni zetu twauziwa.