Omb. 5:1-10 Swahili Union Version (SUV)

1. Ee BWANA, kumbuka yaliyotupata;Utazame na kuiona aibu yetu.

2. Urithi wetu umegeuka kuwa mali ya wageni;Na nyumba zetu kuwa mali ya makafiri.

3. Tumekuwa yatima waliofiwa na baba;Mama zetu wamekuwa kama wajane.

4. Tumekunywa maji yetu kwa fedha;Kuni zetu twauziwa.

5. Watufuatiao wa juu ya shingo zetu;Tumechoka tusipate raha yo yote.

6. Tumewapa hao Wamisri mkono;Na Waashuri nao, ili tushibe chakula.

7. Baba zetu walitenda dhambi hata hawako;Na sisi tumeyachukua maovu yao.

8. Watumwa wanatutawala;Hakuna mtu wa kutuokoa na mikono yao.

9. Twapata chakula kwa kujihatarisha nafsi zetu;Kwa sababu ya upanga wa nyikani.

10. Ngozi yetu ni nyeusi kama tanuu;Kwa sababu ya hari ya njaa ituteketezayo.

Omb. 5