1. Ee BWANA, kumbuka yaliyotupata;Utazame na kuiona aibu yetu.
2. Urithi wetu umegeuka kuwa mali ya wageni;Na nyumba zetu kuwa mali ya makafiri.
3. Tumekuwa yatima waliofiwa na baba;Mama zetu wamekuwa kama wajane.
4. Tumekunywa maji yetu kwa fedha;Kuni zetu twauziwa.
5. Watufuatiao wa juu ya shingo zetu;Tumechoka tusipate raha yo yote.
6. Tumewapa hao Wamisri mkono;Na Waashuri nao, ili tushibe chakula.
7. Baba zetu walitenda dhambi hata hawako;Na sisi tumeyachukua maovu yao.
8. Watumwa wanatutawala;Hakuna mtu wa kutuokoa na mikono yao.
9. Twapata chakula kwa kujihatarisha nafsi zetu;Kwa sababu ya upanga wa nyikani.
10. Ngozi yetu ni nyeusi kama tanuu;Kwa sababu ya hari ya njaa ituteketezayo.