9. Uchafu wake ulikuwa katika marinda yake;Hakukumbuka mwisho wake;Kwa hiyo ameshuka kwa ajabu;Yeye hana mtu wa kumfariji;Tazama, BWANA, teso langu;Maana huyo adui amejitukuza.
10. Huyo mtesi amenyosha mkono wakeJuu ya matamaniko yake yote;Maana ameona ya kuwa makafiri wameingiaNdani ya patakatifu pake;Ambao kwa habari zao wewe uliamuruWasiingie katika kusanyiko lako.
11. Watu wake wote hupiga kite,Wanatafuta chakula;Wameyatoa matamaniko yao wapate chakulaCha kuihuisha nafsi;Ee BWANA, tazama, uangalie;Kwa maana mimi nimekuwa mnyonge.