Mwa. 49:12-15 Swahili Union Version (SUV)

12. Macho yake yatakuwa mekundu kwa mvinyo,Na meno yake yatakuwa meupe kwa maziwa.

13. Zabuloni atakaa pwani ya bahari,Naye atakuwa kama pwani za kuegesha merikebu,Na mpaka wake utakuwa kando ya Sidoni.

14. Isakari ni punda hodari,Ajilazaye kati ya mazizi ya kondoo;

15. Akaona mahali pa raha, kuwa pema,Na nchi, ya kuwa ni nzuri,Akainama bega lake lichukue mizigo,Akawa mtumishi kwa kazi ngumu.

Mwa. 49