46. ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.]
47. Na jicho lako likikukosesha, ling’oe, ulitupe; ni afadhali kuingia katika ufalme wa Mungu, una chongo, kuliko kuwa na macho mawili, na kutupwa katika jehanum;
48. ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.
49. Kwa sababu kila mtu atatiwa chumvi kwa moto.
50. Chumvi ni njema; lakini chumvi ikiwa si chumvi tena, mtaitia nini ikolee? Mwe na chumvi ndani yenu, mkakae kwa amani ninyi kwa ninyi.