1. Mara kulipokuwa asubuhi wakuu wa makuhani walifanya shauri pamoja na wazee na waandishi na baraza nzima, wakamfunga Yesu, wakamchukua, wakamleta mbele ya Pilato.
2. Pilato akamwuliza, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Akajibu, akamwambia, Wewe wasema.
3. Nao wakuu wa makuhani walikuwa wakimshitaki mambo mengi.
4. Pilato akamwuliza tena akisema, Hujibu neno? Tazama ni mambo mangapi wanayokushitaki!
5. Wala Yesu hakujibu neno tena, hata Pilato akastaajabu.
6. Basi wakati wa sikukuu huwafungulia mfungwa mmoja, wamwombaye.
7. Palikuwa na mtu aitwaye Baraba, amefungwa pamoja na watu waliofanya fitina, na kufanya uuaji katika fitina ile.
8. Makutano wakaja, wakaanza kuomba awafanyie kama vile alivyozoea.
9. Pilato akawajibu, akisema, Je! Mnataka niwafungulie mfalme wa Wayahudi?
10. Kwa maana alitambua ya kuwa wakuu wa makuhani wamemtoa kwa husuda.
11. Lakini wakuu wa makuhani wakawataharakisha makutano, kwamba afadhali awafungulie Baraba.
12. Pilato akajibu tena akawaambia, Basi nimtendeje huyu mnayemnena kuwa ni mfalme wa Wayahudi?
13. Wakapiga kelele tena, Msulibishe.