Mk. 14:52-58 Swahili Union Version (SUV)

52. naye akaiacha ile nguo ya kitani, akakimbia yu uchi.

53. Nao wakamchukua Yesu kwa Kuhani Mkuu; wakamkusanyikia wote, wakuu wa makuhani na wazee na waandishi.

54. Naye Petro akamfuata kwa mbali, hata ndani katika behewa ya Kuhani Mkuu; akawa ameketi pamoja na watumishi, anakota moto mwangani.

55. Basi wakuu wa makuhani na baraza yote wakatafuta ushuhuda juu ya Yesu wapate kumwua; wasione.

56. Kwa maana wengi walimshuhudia uongo, walakini ushuhuda wao haukupatana.

57. Hata wengine wakasimama, wakamshuhudia uongo, wakisema,

58. Sisi tulimsikia akisema, Mimi nitalivunja hekalu hili lililofanyika kwa mikono, na katika siku tatu nitajenga jingine lisilofanyika kwa mikono.

Mk. 14