50. Ndipo wakamwacha, wakakimbia wote.
51. Na kijana mmoja alimfuata, amejitanda mwili wake nguo ya kitani; wakamkamata;
52. naye akaiacha ile nguo ya kitani, akakimbia yu uchi.
53. Nao wakamchukua Yesu kwa Kuhani Mkuu; wakamkusanyikia wote, wakuu wa makuhani na wazee na waandishi.
54. Naye Petro akamfuata kwa mbali, hata ndani katika behewa ya Kuhani Mkuu; akawa ameketi pamoja na watumishi, anakota moto mwangani.
55. Basi wakuu wa makuhani na baraza yote wakatafuta ushuhuda juu ya Yesu wapate kumwua; wasione.
56. Kwa maana wengi walimshuhudia uongo, walakini ushuhuda wao haukupatana.
57. Hata wengine wakasimama, wakamshuhudia uongo, wakisema,