50. Ndipo wakamwacha, wakakimbia wote.
51. Na kijana mmoja alimfuata, amejitanda mwili wake nguo ya kitani; wakamkamata;
52. naye akaiacha ile nguo ya kitani, akakimbia yu uchi.
53. Nao wakamchukua Yesu kwa Kuhani Mkuu; wakamkusanyikia wote, wakuu wa makuhani na wazee na waandishi.