Mk. 14:50-53 Swahili Union Version (SUV)

50. Ndipo wakamwacha, wakakimbia wote.

51. Na kijana mmoja alimfuata, amejitanda mwili wake nguo ya kitani; wakamkamata;

52. naye akaiacha ile nguo ya kitani, akakimbia yu uchi.

53. Nao wakamchukua Yesu kwa Kuhani Mkuu; wakamkusanyikia wote, wakuu wa makuhani na wazee na waandishi.

Mk. 14