Mk. 14:49-57 Swahili Union Version (SUV)

49. Kila siku nalikuwa mbele yenu hekaluni nikifundisha, msinikamate; lakini haya yamekuwa ili maandiko yapate kutimia.

50. Ndipo wakamwacha, wakakimbia wote.

51. Na kijana mmoja alimfuata, amejitanda mwili wake nguo ya kitani; wakamkamata;

52. naye akaiacha ile nguo ya kitani, akakimbia yu uchi.

53. Nao wakamchukua Yesu kwa Kuhani Mkuu; wakamkusanyikia wote, wakuu wa makuhani na wazee na waandishi.

54. Naye Petro akamfuata kwa mbali, hata ndani katika behewa ya Kuhani Mkuu; akawa ameketi pamoja na watumishi, anakota moto mwangani.

55. Basi wakuu wa makuhani na baraza yote wakatafuta ushuhuda juu ya Yesu wapate kumwua; wasione.

56. Kwa maana wengi walimshuhudia uongo, walakini ushuhuda wao haukupatana.

57. Hata wengine wakasimama, wakamshuhudia uongo, wakisema,

Mk. 14