Mk. 14:41-47 Swahili Union Version (SUV)

41. Akaja mara ya tatu, akawaambia, Laleni sasa, mpumzike; yatosha, saa imekuja; tazama, Mwana wa Adamu anatiwa mikononi mwao wenye dhambi.

42. Ondokeni, twendeni zetu; tazama, yule anayenisaliti amekaribia.

43. Basi alipokuwa katika kusema, mara Yuda alifika, mmoja wa wale Thenashara, na pamoja naye mkutano, wana panga na marungu, wametoka kwa wakuu wa makuhani, na waandishi, na wazee.

44. Na yule anayemsaliti alikuwa amewapa ishara, akisema, Nitakayembusu, huyo ndiye; mkamateni, mkamchukue salama.

45. Basi alipokuja, mara akamwendea, akasema, Rabi, akambusu.

46. Wakanyosha mikono yao wakamkamata.

47. Na mmoja wao waliokuwapo akafuta upanga, akampiga mtumwa wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.

Mk. 14