Mk. 14:39-53 Swahili Union Version (SUV)

39. Akaenda zake tena, akaomba, akisema neno lilo hilo.

40. Akaja tena akawakuta wamelala, maana macho yao yamekuwa mazito, wala hawakujua la kumjibu.

41. Akaja mara ya tatu, akawaambia, Laleni sasa, mpumzike; yatosha, saa imekuja; tazama, Mwana wa Adamu anatiwa mikononi mwao wenye dhambi.

42. Ondokeni, twendeni zetu; tazama, yule anayenisaliti amekaribia.

43. Basi alipokuwa katika kusema, mara Yuda alifika, mmoja wa wale Thenashara, na pamoja naye mkutano, wana panga na marungu, wametoka kwa wakuu wa makuhani, na waandishi, na wazee.

44. Na yule anayemsaliti alikuwa amewapa ishara, akisema, Nitakayembusu, huyo ndiye; mkamateni, mkamchukue salama.

45. Basi alipokuja, mara akamwendea, akasema, Rabi, akambusu.

46. Wakanyosha mikono yao wakamkamata.

47. Na mmoja wao waliokuwapo akafuta upanga, akampiga mtumwa wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.

48. Yesu akajibu, akawaambia, Je! Ni kama juu ya mnyang’anyi mmetoka wenye panga na marungu, kunitwaa mimi?

49. Kila siku nalikuwa mbele yenu hekaluni nikifundisha, msinikamate; lakini haya yamekuwa ili maandiko yapate kutimia.

50. Ndipo wakamwacha, wakakimbia wote.

51. Na kijana mmoja alimfuata, amejitanda mwili wake nguo ya kitani; wakamkamata;

52. naye akaiacha ile nguo ya kitani, akakimbia yu uchi.

53. Nao wakamchukua Yesu kwa Kuhani Mkuu; wakamkusanyikia wote, wakuu wa makuhani na wazee na waandishi.

Mk. 14