Mk. 14:24-30 Swahili Union Version (SUV)

24. Akawaambia, Hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi.

25. Amin, nawaambia ninyi, Sitakunywa tena kabisa uzao wa mzabibu, hata siku ile nitakapounywa mpya katika ufalme wa Mungu.

26. Nao walipokwisha kuimba walitoka kwenda mlima wa Mizeituni.

27. Yesu akawaambia, Mtakunguwazwa ninyi nyote kwa ajili yangu usiku huu; kwa kuwa imeandikwa,Nitampiga mchungaji, na kondoo watatawanyika.

28. Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.

29. Petro akamwambia, Hata wajapokunguwazwa wote, lakini siyo mimi.

30. Yesu akamwambia, Amin, nakuambia wewe, Leo, usiku huu, kabla ya kuwika jogoo mara mbili, utanikana mara tatu.

Mk. 14