9. Ewe mvivu, utalala hata lini?Utaondoka lini katika usingizi wako?
10. Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo,Bado kukunja mikono upate usingizi!
11. Hivyo umaskini wako huja kama mnyang’anyi,Na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha.
12. Mtu asiyefaa kitu, mtu wa uovu;Huenda njiani mwenye kinywa cha upotofu.
13. Hukonyeza kwa macho, hunena kwa miguu,Huwaashiria watu kwa vidole vyake.
14. Mna upotofu moyoni mwake, hutunga uovu daima,Hupanda mbegu za magomvi.
15. Basi msiba utampata kwa ghafula;Ghafula atavunjika, bila njia ya kupona.
16. Kuna vitu sita anavyovichukia BWANA;Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake.
17. Macho ya kiburi, ulimi wa uongo,Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia;
18. Moyo uwazao mawazo mabaya;Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu;
19. Shahidi wa uongo asemaye uongo;Naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu.
20. Mwanangu, shika maagizo ya baba yako,Wala usiiache sheria ya mama yako.
21. Yafunge hayo katika moyo wako daima;Jivike hayo shingoni mwako.
22. Uendapo yatakuongoza, ulalapo yatakulinda,Na uamkapo yatazungumza nawe.
23. Maana maagizo hayo ni taa, na sheria hiyo ni nuru,Na maonyo ya kumwadilisha mtu ni njia ya uzima.
24. Yakulinde na mwanamke mwovu, asikupate,Na kukuponya na ubembelezi wa mgeni.