12. Mtu asiyefaa kitu, mtu wa uovu;Huenda njiani mwenye kinywa cha upotofu.
13. Hukonyeza kwa macho, hunena kwa miguu,Huwaashiria watu kwa vidole vyake.
14. Mna upotofu moyoni mwake, hutunga uovu daima,Hupanda mbegu za magomvi.
15. Basi msiba utampata kwa ghafula;Ghafula atavunjika, bila njia ya kupona.
16. Kuna vitu sita anavyovichukia BWANA;Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake.
17. Macho ya kiburi, ulimi wa uongo,Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia;
18. Moyo uwazao mawazo mabaya;Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu;
19. Shahidi wa uongo asemaye uongo;Naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu.
20. Mwanangu, shika maagizo ya baba yako,Wala usiiache sheria ya mama yako.
21. Yafunge hayo katika moyo wako daima;Jivike hayo shingoni mwako.
22. Uendapo yatakuongoza, ulalapo yatakulinda,Na uamkapo yatazungumza nawe.
23. Maana maagizo hayo ni taa, na sheria hiyo ni nuru,Na maonyo ya kumwadilisha mtu ni njia ya uzima.
24. Yakulinde na mwanamke mwovu, asikupate,Na kukuponya na ubembelezi wa mgeni.
25. Usiutamani uzuri wake moyoni mwako;Wala usikubali akunase kwa kope za macho yake.
26. Maana kwa malaya mtu hutiwa katika hali ya kuhitaji kipande cha mkate;Na kahaba humwinda mtu anase nafsi yake iliyo ya thamani
27. Je! Mtu aweza kuua moto kifuani pake,Na nguo zake zisiteketezwe?
28. Je! Mtu aweza kukanyaga makaa ya moto,Na nyayo zake zisiungue?
29. Ndivyo alivyo aingiaye kwa mke wa jirani yake;Kila mtu amgusaye huyo atakuwa na hatia.