8. Fumbua kinywa chako kwa ajili yake aliye bubu;Uwatetee watu wote walioachwa peke yao;
9. Fumbua kinywa chako, uhukumu kwa haki;Uwapatie maskini na wahitaji haki yao.
10. Mke mwema, ni nani awezaye kumwona?Maana kima chake chapita kima cha marijani.
11. Moyo wa mumewe humwamini,Wala hatakosa kupata mapato.