Mit. 31:8-11 Swahili Union Version (SUV)

8. Fumbua kinywa chako kwa ajili yake aliye bubu;Uwatetee watu wote walioachwa peke yao;

9. Fumbua kinywa chako, uhukumu kwa haki;Uwapatie maskini na wahitaji haki yao.

10. Mke mwema, ni nani awezaye kumwona?Maana kima chake chapita kima cha marijani.

11. Moyo wa mumewe humwamini,Wala hatakosa kupata mapato.

Mit. 31