6. Mpe kileo yeye aliye karibu na kupotea;Kampe divai yeye aliye na uchungu nafsini.
7. Anywe akausahau umaskini wake;Asiikumbuke tena taabu yake.
8. Fumbua kinywa chako kwa ajili yake aliye bubu;Uwatetee watu wote walioachwa peke yao;
9. Fumbua kinywa chako, uhukumu kwa haki;Uwapatie maskini na wahitaji haki yao.
10. Mke mwema, ni nani awezaye kumwona?Maana kima chake chapita kima cha marijani.
11. Moyo wa mumewe humwamini,Wala hatakosa kupata mapato.
12. Humtendea mema wala si mabaya,Siku zote za maisha yake.
13. Hutafuta sufu na kitani;Hufanya kazi yake ya mikono kwa moyo.