Mit. 31:16-31 Swahili Union Version (SUV)

16. Huangalia shamba, akalinunua;Kwa mapato ya mikono yake hupanda mizabibu.

17. Hujifunga nguvu viunoni kama mshipi;Hutia mikono yake nguvu.

18. Huona kama bidhaa yake ina faida;Taa yake haizimiki usiku.

19. Hutia mikono yake katika kusokota;Na mikono yake huishika pia.

20. Huwakunjulia maskini mikono yake;Naam, huwanyoshea wahitaji mikono yake.

21. Hawahofii theluji watu wa nyumbani mwake;Maana wote wa nyumbani mwake huvikwa nguo nyekundu.

22. Hujifanyia mazulia ya urembo;Mavazi yake ni kitani safi na urujuani.

23. Mume wake hujulikana malangoni;Aketipo pamoja na wazee wa nchi.

24. Hufanya nguo za kitani na kuziuza;Huwapa wafanya biashara mishipi.

25. Nguvu na hadhi ndiyo mavazi yake;Anaucheka wakati ujao.

26. Hufumbua kinywa chake kwa hekima,Na sheria ya wema i katika ulimi wake.

27. Huangalia sana njia za watu wa nyumbani mwake;Wala hali chakula cha uvivu.

28. Wanawe huondoka na kumwita heri;Mumewe naye humsifu, na kusema,

29. Binti za watu wengi wamefanya mema,Lakini wewe umewapita wote.

30. Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili;Bali mwanamke amchaye BWANA, ndiye atakayesifiwa.

31. Mpe mapato ya mikono yake,Na matendo yake yamsifu malangoni.

Mit. 31