14. Afanana na merikebu za biashara;Huleta chakula chake kutoka mbali.
15. Tena huamka, kabla haujaisha usiku;Huwapa watu wa nyumbani mwake chakula;Na wajakazi wake sehemu zao.
16. Huangalia shamba, akalinunua;Kwa mapato ya mikono yake hupanda mizabibu.
17. Hujifunga nguvu viunoni kama mshipi;Hutia mikono yake nguvu.
18. Huona kama bidhaa yake ina faida;Taa yake haizimiki usiku.
19. Hutia mikono yake katika kusokota;Na mikono yake huishika pia.
20. Huwakunjulia maskini mikono yake;Naam, huwanyoshea wahitaji mikono yake.
21. Hawahofii theluji watu wa nyumbani mwake;Maana wote wa nyumbani mwake huvikwa nguo nyekundu.
22. Hujifanyia mazulia ya urembo;Mavazi yake ni kitani safi na urujuani.
23. Mume wake hujulikana malangoni;Aketipo pamoja na wazee wa nchi.
24. Hufanya nguo za kitani na kuziuza;Huwapa wafanya biashara mishipi.
25. Nguvu na hadhi ndiyo mavazi yake;Anaucheka wakati ujao.