Mit. 31:13-18 Swahili Union Version (SUV)

13. Hutafuta sufu na kitani;Hufanya kazi yake ya mikono kwa moyo.

14. Afanana na merikebu za biashara;Huleta chakula chake kutoka mbali.

15. Tena huamka, kabla haujaisha usiku;Huwapa watu wa nyumbani mwake chakula;Na wajakazi wake sehemu zao.

16. Huangalia shamba, akalinunua;Kwa mapato ya mikono yake hupanda mizabibu.

17. Hujifunga nguvu viunoni kama mshipi;Hutia mikono yake nguvu.

18. Huona kama bidhaa yake ina faida;Taa yake haizimiki usiku.

Mit. 31