13. Hutafuta sufu na kitani;Hufanya kazi yake ya mikono kwa moyo.
14. Afanana na merikebu za biashara;Huleta chakula chake kutoka mbali.
15. Tena huamka, kabla haujaisha usiku;Huwapa watu wa nyumbani mwake chakula;Na wajakazi wake sehemu zao.
16. Huangalia shamba, akalinunua;Kwa mapato ya mikono yake hupanda mizabibu.
17. Hujifunga nguvu viunoni kama mshipi;Hutia mikono yake nguvu.
18. Huona kama bidhaa yake ina faida;Taa yake haizimiki usiku.