Mit. 31:12-15 Swahili Union Version (SUV)

12. Humtendea mema wala si mabaya,Siku zote za maisha yake.

13. Hutafuta sufu na kitani;Hufanya kazi yake ya mikono kwa moyo.

14. Afanana na merikebu za biashara;Huleta chakula chake kutoka mbali.

15. Tena huamka, kabla haujaisha usiku;Huwapa watu wa nyumbani mwake chakula;Na wajakazi wake sehemu zao.

Mit. 31