Mit. 30:26-33 Swahili Union Version (SUV)

26. Wibari ni watu dhaifu;Lakini hujifanyia nyumba katika miamba.

27. Nzige hawana mfalme;Lakini huenda wote pamoja vikosi vikosi.

28. Mjusi hushika kwa mikono yake;Lakini yumo majumbani mwa wafalme.

29. Kuna watatu wenye mwendo wa kupendeza,Naam, wanne walio na mwendo mzuri.

30. Simba aliye hodari kupita wanyama wote;Wala hajiepushi na aliye yote;

31. Jimbi aendaye tambo; na beberu;Na mfalme ambaye haasiki.

32. Ikiwa umefanya kipumbavu kwa kujikuza;Au ikiwa umewaza mabaya;Basi weka mkono wako juu ya kinywa chako.

33. Kwa maana kupiga maziwa huleta siagi;Na kupiga pua hutokeza damu;kadhalika kuchochea hasira hutokeza ugomvi.

Mit. 30