Mit. 30:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Maneno ya Aguri bin Yake; mausia mtu huyu aliyomwambia Ithieli, naam, Ithieli na Ukali.

2. Hakika nimekuwa kama mnyama, wala si mtu;Wala sina ufahamu wa mwanadamu;

3. Wala sikujifunza hekima;Wala sina maarifa ya kumjua Mtakatifu.

4. Ni nani aliyepanda mbinguni na kushuka chini?Ni nani aliyekamata upepo kwa makonzi yake?Ni nani aliyeyafunga maji ndani ya nguo yake?Ni nani aliyefanya imara ncha zote za nchi?Jina lake ni nani? Na ni nani jina la mwanawe, kama wajua?

Mit. 30