1. Waovu hukimbia wasipofuatiwa na mtu;Bali wenye haki ni wajasiri kama simba.
2. Kwa sababu ya maasi ya nchi wakuu wake huwa wengi;Bali kwa wenye ufahamu na maarifa hali ya nchi hudumishwa
3. Mtu mhitaji awaoneaye maskini,Ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza chakula.
4. Wao waiachao sheria huwasifu waovu;Bali wao waishikao hushindana nao.
5. Watu wabaya hawaelewi na hukumu;Bali wamtafutao BWANA huelewa na yote.
6. Afadhali maskini aendaye katika unyofu wake,Kuliko mpotofu wa njia angawa ni tajiri.
7. Yeye aishikaye sheria ni mwana mwenye hekima;Bali aliye rafiki wa walafi humwaibisha babaye.
8. Yeye azidishaye mali yake kwa riba na faida,Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.
9. Yeye aligeuzaye sikio lake asiisikie sheria,Hata sala yake ni chukizo.
10. Kila mtu awapotezaye wenye haki katika njia mbaya,Ataanguka katika rima lake mwenyewe;Bali wakamilifu watarithi mema.