Mit. 23:17-30 Swahili Union Version (SUV)

17. Moyo wako usiwahusudu wenye dhambi;Bali mche BWANA mchana kutwa;

18. Maana bila shaka iko thawabu;Na tumaini lako halitabatilika.

19. Sikia, mwanangu, uwe na hekima,Na kuuongoza moyo wako katika njia njema.

20. Usiwe miongoni mwao wanywao mvinyo;Miongoni mwao walao nyama kwa pupa.

21. Kwa maana mlevi na mlafi huingia umaskini,Na utepetevu humvika mtu nguo mbovu.

22. Msikilize baba yako aliyekuzaa,Wala usimdharau mama yako akiwa mzee.

23. Inunue kweli, wala usiiuze;Naam, hekima, na mafundisho, na ufahamu.

24. Baba yake mwenye haki atashangilia;Naye amzaaye mtoto mwenye hekima atamfurahia.

25. Na wafurahi baba yako na mama yako;Na afurahi aliyekuzaa.

26. Mwanangu, nipe moyo wako;Macho yako yapendezwe na njia zangu.

27. Kwa maana kahaba ni shimo refu;Na malaya ni rima jembamba.

28. Naam, huotea kama mnyang’anyi;Huwaongeza wenye hila katika wanadamu.

29. Ni nani apigaye, Yowe? Ni nani aliaye, Ole?Ni nani mwenye ugomvi? Ni nani mwenye mguno?Ni nani aliye na jeraha zisizo na sababu?Ni nani aliye na macho mekundu?

30. Ni wale wakaao sana kwenye mvinyo;Waendao kutafuta divai iliyochanganyika.

Mit. 23