Mit. 21:10-24 Swahili Union Version (SUV)

10. Nafsi ya mtu mbaya hutamani uovu;Jirani yake hapati fadhili machoni pake.

11. Mwenye mzaha aadhibiwapo, mjinga hupata hekima;Na mwenye hekima afundishwapo, hupokea maarifa.

12. Mwenye haki huitafakari nyumba ya mtu mbaya;Jinsi wabaya waangushwavyo wakaangamia.

13. Azibaye masikio yake asisikie kilio cha maskini,Yeye naye atalia, lakini hatasikiwa.

14. Kipawa cha siri hutuliza hasira;Na rushwa bindoni humliza ghadhabu kali.

15. Ni furaha yao wenye haki kutenda hukumu;Lakini ni uharibifu kwao watendao maovu.

16. Mtu aikosaye njia ya busaraAtakaa katika mkutano wao waliokufa.

17. Mtu apendaye anasa atakuwa maskini;Apendaye mvinyo na mafuta hatakuwa tajiri.

18. Mtu asiye haki ni fidia ya wenye haki;Naye afanyaye hila ni badala ya watu wa adili.

19. Ni afadhali kukaa katika nchi ya nyika;Kuliko na mwanamke mgomvi, mchokozi.

20. Kuna hazina ya thamani na mafuta katika maskani ya mwenye hekima;Bali mwanadamu aliye mpumbavu huyameza.

21. Aandamaye haki na fadhili,Ataona uhai na haki na heshima.

22. Mwenye hekima huupandia mji wao wenye nguvu;Na kuziangusha nguvu za tumaini lao.

23. Mtu azuiaye kinywa chake na ulimi wake,Atajilinda nafsi yake na taabu.

24. Mwenye kiburi na kutakabari, jina lake ni mbishi;Hutenda mambo katika majivuno ya kiburi chake.

Mit. 21