30. Moyo ulio mzima ni uhai wa mwili;Bali husuda ni ubovu wa mifupa.
31. Amwoneaye maskini humsuta Muumba wake;Bali yeye awahurumiaye wahitaji humheshimu.
32. Mtu mbaya husukumwa chini katika kutenda mabaya kwake;Bali mwenye haki ana matumaini katika kufa kwake.
33. Hekima hukaa katika moyo wake mwenye ufahamu;Bali yaliyo ndani ya wapumbavu hudhihirika.
34. Haki huinua taifa;Bali dhambi ni aibu ya watu wo wote.