Mit. 14:30-34 Swahili Union Version (SUV)

30. Moyo ulio mzima ni uhai wa mwili;Bali husuda ni ubovu wa mifupa.

31. Amwoneaye maskini humsuta Muumba wake;Bali yeye awahurumiaye wahitaji humheshimu.

32. Mtu mbaya husukumwa chini katika kutenda mabaya kwake;Bali mwenye haki ana matumaini katika kufa kwake.

33. Hekima hukaa katika moyo wake mwenye ufahamu;Bali yaliyo ndani ya wapumbavu hudhihirika.

34. Haki huinua taifa;Bali dhambi ni aibu ya watu wo wote.

Mit. 14