Mit. 14:23-31 Swahili Union Version (SUV)

23. Katika kila kazi mna faida;Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.

24. Taji ya wenye hekima ni mali zao;Bali upumbavu wa wajinga ni upumbavu tu.

25. Shahidi wa kweli huponya nafsi za watu;Bali atoaye uongo hudanganya.

26. Kumcha BWANA ni tumaini imara;Watoto wake watakuwa na kimbilio.

27. Kumcha BWANA ni chemchemi ya uzima,Ili kuepukana na tanzi za mauti.

28. Utukufu wa mfalme ni wingi wa watu wake;Bali uchache wa watu ni uharibifu wa mkuu wao.

29. Asiye mwepesi wa hasira ana fahamu nyingi;Bali mwenye roho ya hamaki hutukuza upumbavu.

30. Moyo ulio mzima ni uhai wa mwili;Bali husuda ni ubovu wa mifupa.

31. Amwoneaye maskini humsuta Muumba wake;Bali yeye awahurumiaye wahitaji humheshimu.

Mit. 14