Mit. 14:22-28 Swahili Union Version (SUV)

22. Je! Hawakosi wawazao mabaya?Bali fadhili na kweli zina wao wawazao mema.

23. Katika kila kazi mna faida;Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.

24. Taji ya wenye hekima ni mali zao;Bali upumbavu wa wajinga ni upumbavu tu.

25. Shahidi wa kweli huponya nafsi za watu;Bali atoaye uongo hudanganya.

26. Kumcha BWANA ni tumaini imara;Watoto wake watakuwa na kimbilio.

27. Kumcha BWANA ni chemchemi ya uzima,Ili kuepukana na tanzi za mauti.

28. Utukufu wa mfalme ni wingi wa watu wake;Bali uchache wa watu ni uharibifu wa mkuu wao.

Mit. 14