22. Je! Hawakosi wawazao mabaya?Bali fadhili na kweli zina wao wawazao mema.
23. Katika kila kazi mna faida;Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.
24. Taji ya wenye hekima ni mali zao;Bali upumbavu wa wajinga ni upumbavu tu.
25. Shahidi wa kweli huponya nafsi za watu;Bali atoaye uongo hudanganya.
26. Kumcha BWANA ni tumaini imara;Watoto wake watakuwa na kimbilio.
27. Kumcha BWANA ni chemchemi ya uzima,Ili kuepukana na tanzi za mauti.
28. Utukufu wa mfalme ni wingi wa watu wake;Bali uchache wa watu ni uharibifu wa mkuu wao.