2. Yeye aendaye kwa unyofu wake humcha BWANA;Bali aliye mkaidi katika njia zake humdharau.
3. Katika kinywa cha mpumbavu mna fimbo ya kiburi,Bali midomo ya wenye hekima huwahifadhi.
4. Zizi ni safi ambapo hapana ng’ombe;Bali nguvu za ng’ombe zaleta faida nyingi.
5. Shahidi mwaminifu hatasema uongo;Bali shahidi wa uongo, pumzi zake ni uongo.
6. Mwenye dharau hutafuta hekima, asiipate;Bali maarifa huwa mepesi kwa mwenye ufahamu.
7. Toka mbele ya uso wa mpumbavu,Maana hutaona kwake midomo ya maarifa.
8. Akili za mwenye busara ni kujua njia yake;Lakini upumbavu wa wapumbavu ni udanganyifu.
9. Wapumbavu huidharau hatia;Bali upo upendeleo kwa wenye haki.
10. Moyo huujua uchungu wa nafsi yake,Wala mgeni haishiriki furaha yake.
11. Nyumba ya mtu mbaya itabomolewa;Bali hema ya mwenye haki itafanikiwa.
12. Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu,Lakini mwisho wake ni njia za mauti.
13. Hata wakati wa kucheka moyo huwa na huzuni;Na mwisho wa furaha ni uzito wa moyo.