18. Wajinga hurithi upumbavu;Bali wenye busara huvikwa taji ya maarifa.
19. Wabaya huinama mbele ya wema,Na wasio haki malangoni mwao wenye haki.
20. Maskini huchukiwa hata na jirani yake;Bali tajiri ana rafiki wengi.
21. Amdharauye mwenzake afanya dhambi;Bali amhurumiaye maskini ana heri.
22. Je! Hawakosi wawazao mabaya?Bali fadhili na kweli zina wao wawazao mema.
23. Katika kila kazi mna faida;Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.