Mit. 14:18-23 Swahili Union Version (SUV)

18. Wajinga hurithi upumbavu;Bali wenye busara huvikwa taji ya maarifa.

19. Wabaya huinama mbele ya wema,Na wasio haki malangoni mwao wenye haki.

20. Maskini huchukiwa hata na jirani yake;Bali tajiri ana rafiki wengi.

21. Amdharauye mwenzake afanya dhambi;Bali amhurumiaye maskini ana heri.

22. Je! Hawakosi wawazao mabaya?Bali fadhili na kweli zina wao wawazao mema.

23. Katika kila kazi mna faida;Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.

Mit. 14