16. Mwenye hekima huogopa, akajitenga na uovu;Bali mpumbavu ana ufidhuli, na kujitumai.
17. Yeye aonaye hasira upesi atatenda kwa ujinga;Na mtu mwenye hila mbaya huzirwa.
18. Wajinga hurithi upumbavu;Bali wenye busara huvikwa taji ya maarifa.
19. Wabaya huinama mbele ya wema,Na wasio haki malangoni mwao wenye haki.
20. Maskini huchukiwa hata na jirani yake;Bali tajiri ana rafiki wengi.
21. Amdharauye mwenzake afanya dhambi;Bali amhurumiaye maskini ana heri.
22. Je! Hawakosi wawazao mabaya?Bali fadhili na kweli zina wao wawazao mema.
23. Katika kila kazi mna faida;Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.
24. Taji ya wenye hekima ni mali zao;Bali upumbavu wa wajinga ni upumbavu tu.
25. Shahidi wa kweli huponya nafsi za watu;Bali atoaye uongo hudanganya.