Mit. 14:16-25 Swahili Union Version (SUV)

16. Mwenye hekima huogopa, akajitenga na uovu;Bali mpumbavu ana ufidhuli, na kujitumai.

17. Yeye aonaye hasira upesi atatenda kwa ujinga;Na mtu mwenye hila mbaya huzirwa.

18. Wajinga hurithi upumbavu;Bali wenye busara huvikwa taji ya maarifa.

19. Wabaya huinama mbele ya wema,Na wasio haki malangoni mwao wenye haki.

20. Maskini huchukiwa hata na jirani yake;Bali tajiri ana rafiki wengi.

21. Amdharauye mwenzake afanya dhambi;Bali amhurumiaye maskini ana heri.

22. Je! Hawakosi wawazao mabaya?Bali fadhili na kweli zina wao wawazao mema.

23. Katika kila kazi mna faida;Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.

24. Taji ya wenye hekima ni mali zao;Bali upumbavu wa wajinga ni upumbavu tu.

25. Shahidi wa kweli huponya nafsi za watu;Bali atoaye uongo hudanganya.

Mit. 14