Mit. 14:12-31 Swahili Union Version (SUV)

12. Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu,Lakini mwisho wake ni njia za mauti.

13. Hata wakati wa kucheka moyo huwa na huzuni;Na mwisho wa furaha ni uzito wa moyo.

14. Ageukaye moyoni hushiba njia zake mwenyewe;Na mtu mwema ataridhika nafsini mwake.

15. Mjinga huamini kila neno;Bali mwenye busara huangalia sana aendavyo.

16. Mwenye hekima huogopa, akajitenga na uovu;Bali mpumbavu ana ufidhuli, na kujitumai.

17. Yeye aonaye hasira upesi atatenda kwa ujinga;Na mtu mwenye hila mbaya huzirwa.

18. Wajinga hurithi upumbavu;Bali wenye busara huvikwa taji ya maarifa.

19. Wabaya huinama mbele ya wema,Na wasio haki malangoni mwao wenye haki.

20. Maskini huchukiwa hata na jirani yake;Bali tajiri ana rafiki wengi.

21. Amdharauye mwenzake afanya dhambi;Bali amhurumiaye maskini ana heri.

22. Je! Hawakosi wawazao mabaya?Bali fadhili na kweli zina wao wawazao mema.

23. Katika kila kazi mna faida;Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.

24. Taji ya wenye hekima ni mali zao;Bali upumbavu wa wajinga ni upumbavu tu.

25. Shahidi wa kweli huponya nafsi za watu;Bali atoaye uongo hudanganya.

26. Kumcha BWANA ni tumaini imara;Watoto wake watakuwa na kimbilio.

27. Kumcha BWANA ni chemchemi ya uzima,Ili kuepukana na tanzi za mauti.

28. Utukufu wa mfalme ni wingi wa watu wake;Bali uchache wa watu ni uharibifu wa mkuu wao.

29. Asiye mwepesi wa hasira ana fahamu nyingi;Bali mwenye roho ya hamaki hutukuza upumbavu.

30. Moyo ulio mzima ni uhai wa mwili;Bali husuda ni ubovu wa mifupa.

31. Amwoneaye maskini humsuta Muumba wake;Bali yeye awahurumiaye wahitaji humheshimu.

Mit. 14