12. Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu,Lakini mwisho wake ni njia za mauti.
13. Hata wakati wa kucheka moyo huwa na huzuni;Na mwisho wa furaha ni uzito wa moyo.
14. Ageukaye moyoni hushiba njia zake mwenyewe;Na mtu mwema ataridhika nafsini mwake.
15. Mjinga huamini kila neno;Bali mwenye busara huangalia sana aendavyo.
16. Mwenye hekima huogopa, akajitenga na uovu;Bali mpumbavu ana ufidhuli, na kujitumai.
17. Yeye aonaye hasira upesi atatenda kwa ujinga;Na mtu mwenye hila mbaya huzirwa.
18. Wajinga hurithi upumbavu;Bali wenye busara huvikwa taji ya maarifa.
19. Wabaya huinama mbele ya wema,Na wasio haki malangoni mwao wenye haki.
20. Maskini huchukiwa hata na jirani yake;Bali tajiri ana rafiki wengi.
21. Amdharauye mwenzake afanya dhambi;Bali amhurumiaye maskini ana heri.
22. Je! Hawakosi wawazao mabaya?Bali fadhili na kweli zina wao wawazao mema.
23. Katika kila kazi mna faida;Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.
24. Taji ya wenye hekima ni mali zao;Bali upumbavu wa wajinga ni upumbavu tu.
25. Shahidi wa kweli huponya nafsi za watu;Bali atoaye uongo hudanganya.
26. Kumcha BWANA ni tumaini imara;Watoto wake watakuwa na kimbilio.
27. Kumcha BWANA ni chemchemi ya uzima,Ili kuepukana na tanzi za mauti.
28. Utukufu wa mfalme ni wingi wa watu wake;Bali uchache wa watu ni uharibifu wa mkuu wao.
29. Asiye mwepesi wa hasira ana fahamu nyingi;Bali mwenye roho ya hamaki hutukuza upumbavu.
30. Moyo ulio mzima ni uhai wa mwili;Bali husuda ni ubovu wa mifupa.
31. Amwoneaye maskini humsuta Muumba wake;Bali yeye awahurumiaye wahitaji humheshimu.