11. Nyumba ya mtu mbaya itabomolewa;Bali hema ya mwenye haki itafanikiwa.
12. Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu,Lakini mwisho wake ni njia za mauti.
13. Hata wakati wa kucheka moyo huwa na huzuni;Na mwisho wa furaha ni uzito wa moyo.
14. Ageukaye moyoni hushiba njia zake mwenyewe;Na mtu mwema ataridhika nafsini mwake.
15. Mjinga huamini kila neno;Bali mwenye busara huangalia sana aendavyo.
16. Mwenye hekima huogopa, akajitenga na uovu;Bali mpumbavu ana ufidhuli, na kujitumai.
17. Yeye aonaye hasira upesi atatenda kwa ujinga;Na mtu mwenye hila mbaya huzirwa.
18. Wajinga hurithi upumbavu;Bali wenye busara huvikwa taji ya maarifa.
19. Wabaya huinama mbele ya wema,Na wasio haki malangoni mwao wenye haki.
20. Maskini huchukiwa hata na jirani yake;Bali tajiri ana rafiki wengi.