1. Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake;Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
2. Yeye aendaye kwa unyofu wake humcha BWANA;Bali aliye mkaidi katika njia zake humdharau.
3. Katika kinywa cha mpumbavu mna fimbo ya kiburi,Bali midomo ya wenye hekima huwahifadhi.
4. Zizi ni safi ambapo hapana ng’ombe;Bali nguvu za ng’ombe zaleta faida nyingi.
5. Shahidi mwaminifu hatasema uongo;Bali shahidi wa uongo, pumzi zake ni uongo.
6. Mwenye dharau hutafuta hekima, asiipate;Bali maarifa huwa mepesi kwa mwenye ufahamu.
7. Toka mbele ya uso wa mpumbavu,Maana hutaona kwake midomo ya maarifa.
8. Akili za mwenye busara ni kujua njia yake;Lakini upumbavu wa wapumbavu ni udanganyifu.
9. Wapumbavu huidharau hatia;Bali upo upendeleo kwa wenye haki.