1. Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake;Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
2. Yeye aendaye kwa unyofu wake humcha BWANA;Bali aliye mkaidi katika njia zake humdharau.
3. Katika kinywa cha mpumbavu mna fimbo ya kiburi,Bali midomo ya wenye hekima huwahifadhi.
4. Zizi ni safi ambapo hapana ng’ombe;Bali nguvu za ng’ombe zaleta faida nyingi.